WENZA WA VIONGOZI WASHAURIWA KUANZISHA BUSTANI ZA NYUMBANI
Na. Dennis Gondwe, NZUGUNI
WENZA
wa viongozi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameshauriwa kuanzisha bustani
za nyumbani ili kusaidia familia zao na wageni wanaowatembelea.
![]() |
Afisa Kilimo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Lucy Kway |
Kauli
hiyo ilitolewa na Afisa Kilimo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Lucy Kway
alipokuwa akiongelea umuhimu wa bustani za nyumbani kwa wenza wa viongozi wa
Halmashauri ya Jiji la Dodoma alipokuwa akihamasisha kilimo cha bustani hizo
kwenye Banda la Jiji la Dodoma katika viwanja vya Nanenane Nzuguni.
Kway
alisema “nichukue nafasi hii kuwashauri wenza wa viongozi katika Halmashauri ya
Jiji la Dodoma kulima bustani za nyumbani kwa ajili ya kusaidia familia zao na
wageni wanaowatembelea. Hii ni muhimu kwa sababu wenza wa viongozi ni mfano wa
kuigwa katika jamii hivyo ni rahisi kwa watu kuiga mfano mzuri kutoka kwa wenza
wa viongozi hapa Halmashauri ya Jiji la Dodoma”.
Akiongelea
kilimo hicho kwa wananchi na watumishi wanaohamia Makao Makuu Dodoma alisema
kuwa bustani hizo ni muhimu kwao. Bustani za nyumbani mtu yeyote anaweza kulima
kwa muda wowote. Kinachotakiwa ni kulima bustani ndogo inayokuwezesha kujikimu
kwa mboga na kuuza. “Kilimo hiki kina faida ya kumpatia mtu kipato. Faida
nyingine ni mtu analima mwenyewe na kuondokana na hatari ya kutumia madawa
zaidi kwenye mboga. Mtu anaweza kulima na kupata fedha za kujikimu au kuuza”
alisema Kway.
Kwa
upande wa Mkazi wa Dodoma Leila Shati aliyetembelea banda la halmashauri ya
jiji la Dodoma alisema kuwa amevutiwa na kilimo cha bustani za nyumbani. Kilimo
hiko ni kama urembo wa nyumbani lakini kina umuhimu mkubwa kwa jamii. “Sisi
wakina mama kilimo hiki ni suluhisho la mbogamboga nyumbani kwa sababu unalima
eneo dogo kwa mpangilio mzuri na kuwa na uhakika wa mboga” alisema Shati.
Maonesho
ya shughuli za wakulima Nanenane mwaka 2023 yanaongozwa na kaulimbiu isemayo
“Vijana na wanawake ni msingi imara wa mifumo endelevu ya chakula”.
MWISHO
Comments
Post a Comment