JIJI LA DODOMA LAJA NA TEKNOLOJIA YA NISHATI MBADALA MAONESHO YA NANENANE

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeanzisha teknolojia ya nishati mbadala ili kuondoa matumizi ya kuni na mkaa kwa wakazi wa mikoa ya kanda ya kati.

Afisa Mifugo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, George Joram


Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Mifugo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, George Joram alipokuwa akiongelea teknolojia ya nishati mbadala inayooneshwa katika banda la mifugo Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Joram alisema “safari hii tumekuja na teknolojia ya nishati mbadala. Tunazalisha gesi kwa kutumia kinyesi cha ng’ombe. Kinyesi cha ng’ombe tunakikusanya kutoka kwenye banda la ng’ombe tunachanganya kwa mchanganyo wa moja kwa moja. Tunachukua kinyesi cha ng’ombe kwenye ndoo ya lita 20 na maji lita 20 tunachanganya na kuzalisha gesi”.

Alisema kuwa baada ya saa 24 bacteria wanazalisha gesi inayoitwa Methane. “Badala ya kutumia mkaa na nishati nyingine kama kuni, unaweza kutumia nishati mbadala ya kutumia gesi ya kinyesi cha mifugo na kulinda na kutunza mazingira. Karibuni sana Banda la Mifugo la Halmashauri ya Jiji la Dodoma mjionee wenyewe mambo ni motomoto” alisema Joram kwa furaha.

Maonesho ya shughuli za wakulima Nanenane mwaka 2023 yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Vijana na wanawake ni msingi imara wa mifumo endelevu ya chakula”.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma