Dkt. Mashinji: Tuimarishe Ubunifu wa Kilimo cha Zabibu Dodoma

              

Na. Leah Mabalwe, DODOMA

Mkuu wa Wilaya ya Manyoni, Dkt. Vincent Mashinji amewataka maafisa kilimo wa Jiji la Dodoma kuongeza juhudi na ubunifu katika kukuza kilimo cha zabibu, kilimo ambacho ni uti wa mgongo wa uchumi wa Jiji la Dodoma.


Hayo aliyasema mara baada ya kutembelea banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika maonesho ya kilimo Nanenane, ambapo alipata fursa ya kuona bidhaa mbalimbali zinazotokana na zabibu, ikiwemo juisi, divai na zabibu kavu.

Alisema kuwa pamoja na jitihada zinazofanyika, bado kuna nafasi kubwa ya kuboresha na kuongeza thamani katika zao hilo. Jiji la Dodoma lina nafasi kubwa ya kuwa kitovu cha zabibu Afrika Mashariki. Kwa upande wenu nyie maafisa kilimo mnapaswa kuwa wabunifu zaidi na hata kufuata zile kanuni ambazo zao hili la zabibu linapaswa kuwa hasa katika hatua ya upandaji” alisema Dkt. Mashinji.

Kwa upande wake Afisa Kilimo Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Emmanuel Mayyo alisema kuwa ujio wa kiongozi huyo ni wa kutia moyo na ni uthibitisho kuwa sekta ya kilimo, hasa zao la zabibu, linamchango mkubwa katika maendeleo ya kiuchumi katika Jiji la Dodoma. Tunamshukuru sana Dkt. Mashinji kwa kututembelea na kutupa maneno ya kututia nguvu. Na hii inaonesha kuwa juhudi zetu zinaonekana. Kama maafisa kilimo wa Jiji la Dodoma, tutaendelea kufanya kazi kwa bidii kuhakikisha Dodoma inabaki kuwa kinara katika uzalishaji bora wa zabibu nchini na taifa kwa ujumla” alisema Mayyo.

MWISHO

Imehaririwa na Nancy Kivuyo

Comments

Popular Posts

Jiji la Dodoma lapewa angalizo lishe bora kwa wananchi

RC Dodoma apongeza wafugaji kwa ushiriki wa Paredi ya Mifugo

Rais Samia: Tumieni kikamilifu Miundombinu, Teknolojia na mitaji iliyowekezwa katika Kilimo, Uvuvi na Mifugo