Vipando bustani vya Jiji la Dodoma yamvutia DC, Dkt. Mashinji
Na. Nancy
Kivuyo, DODOMA
Mkuu
wa Wilaya ya Manyoni, Dkt. Vincent
Mashinji ametembelea banda la vipando bustani ya mbogamboga la
Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kujionea aina mbalimbali za mboga na matunda
zilizoandaliwa kwaajili ya kutolea elimu na kuhamasisha wananchi kuzingatia mlo
kamili.
Teknolojia
hizo za kisasa zinawezesha mbogamboga kupandwa kwenye vitu mbalimbali kama
kiroba, kopo la maji au eneo dogo kutokana na ufinyu wa maeneo na zikaendelea
kustawi kwa ubora unaotakiwa.
Baada ya
kupewa maelezo ya kina kuhusiana na aina mbalimbali za teknolojia ya upandaji
wa mbogamboga alisema
kuwa anawapongeza wataalam kwa kubuni njia za kisasa za
kuhakikisha wananchi wanakuwa na afya njema. “Hiki kilimo
cha mjini mnapaswa kukiangalia kwa jicho la ziada kwa kuhakikisha mnatoa elimu
nzuri zaidi, lakini pia mshirikiane na watu wa mipango miji ili kuhakikisha
watu wanapata maeneo mazuri yenye nafasi ya kufanya hiki mnachowaelekeza” alisema Dkt. Mashinji.
Kwa
upande wake Afisa Kilimo Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Emmanuel Mayyo alisema kuwa vipando
bustani vya kisasa vina faida kubwa kwa walaji wa mboga za majani kwasababu
wanaimarisha afya na kuondoa hatari ya magonjwa nyemelezi. “Ni muhimu sana katika mlo wa kila siku kuwa na mboga
za majani na matunda, wananchi waje wajielimishe ili wakapande mboga kwenye
maeneo yao hata kwa udogo hivyo hivyo. Kila mboga ina faida zake mwilini kwa
maana hiyo tukizingatia hilo tutatengeneza afya zetu muda wote na kuepuka
maradhi nyemelezi yanayotakana na kukosa virutubisho muhimu mwilini” alisema Mayyo.
Alimalizia kwa
kuwaalika wananchi wote kutembelea vipando bustani vya halmashauri ili
kujifunza namna ya kupanda mboga mboga na matunda katika eneo dogo.
“Nawakaribisha sana watu wote katika banda letu. Tuna teknolojia za kisasa
ambazo zinawezesha hata mtu anayeishi nyumba ya kupanga kuwa na namna ya kupata
mboga za majani muda wote. Kwasasa kwa ubunifu wa njia hizi nafuu, kukosa mboga
za majani katika mlo ni mtu ajitakie mwenyewe” alimaliza Mayyo.
MWISHO
Comments
Post a Comment