Mtoto wa kike apewe fursa ya kuongoza
Na. Faraja Mbise, DODOMA
Kuelekea
kilele cha maadhimisho ya siku ya mtoto wa kike Duniani, ambayo hufanyika kila
mwaka Oktoba 11, jamii imeaswa kumshirikisha mtoto wa kike katika ngazi ya
uongozi tangu anapoanza kukua mpaka anapokuwa mtu mzima.
Hayo
yalisemwa na Mkurugenzi wa taasisi ya Msichana Initiatives, Rebecca Gyumi alipokuwa
akizungumza na wananchi wa Kata ya Lamaiti, Tarafa ya Mndemu, Wilaya ya Bahi, Mkoa
wa Dodoma katika Tamasha la Msichana Amani Music Festival.
“Siku
hii katika nchi yetu, tunaongozwa na kaulimbiu ya Msichana na Uongozi,
Mshirikishe Wakati ni Sasa. Kupitia jukwaa letu la Agenda ya Msichana, tumeitohoa
zaidi kaulimbiu yetu ya kitaifa ambapo tunasema Msichana na uongozi, kwakutumia
Fursa za Kidijitali au teknolojia ya kidijitali, kwa maana ya kuangalia namna
wasichana wanavyoweza kuonesha uongozi kupitia fursa mbalimbali zinazopatikana
kwenye teknolojia ya kidigitali” alisema Gyumi.
Wakati
akizungumza na kundi la wananchi na watoto wa kike alisema kuwa, katika kipindi
hicho ambacho nchi inaelekea katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu
wa Rais, Wabunge na Madiwani ni vizuri kumshirikisha mtoto wa kike katika
masuala ya uongozi kwa kuanza pindi tu wawapo shuleni na kwenye klabu
zinazohusu masuala ya kijamii.
Kutokana
na ripoti ya Jeshi la Polisi nchini Tanzania, inaonesha mwaka 2023 kulikuwa na
matukio ya ukatili kwa watoto takribani 15,000 ambayo ukilinganisha na mwaka
2022 matukio yalikuwa 12,000. Kwahiyo, ni sawa na ongezeko la asilimia 25, na
makosa hayo unapoyachambua ni makosa ya ubakaji 8,000, ulawiti 2,300 na mimba 1,400.
Gyumi
alibainisha changamoto hizo ambazo wanakumbana nazo katika harakati za
kumkomboa mtoto wa kike katika wimbi la ukatili wa kijinsia, ambalo ndio
changamoto kubwa inayompelekea mtoto wa kike kushindwa kutimiza ndoto zake na
kutoa rai kwa jamii kuwalinda watoto wa kike na ukatili wa kijinsia.
“Tukizungumza
kuhusiana na masuala ambayo yanamfanya mtoto wa kike ashindwe kuwa kiongozi,
hatuwezi kuacha kuzungumzia tamaduni, mila na desturi kandamizi. Kwasababu
hatuwezi kuzungumza mtoto wa kike kuwa kiongozi wakati anaozeshwa akiwa na umri
wa miaka 12” alisisitiza Gyumi kwa uchungu.
Aidha,
alitoa takwimu ya Sensa ya Wat una Makazi ya mwaka 2022 inayoonesha kuwa watoto
wa Tanzania ni nusu ya wananchi wote takribani Milioni 29 na kati yao milioni
14 ni watoto wa kike.
Akizungumza
kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Afisa Tarafa ya Mndemu, Isaya Matata, aliishauri
jamii kumshirikisha mtoto wa kike katika kumuelimisha stadi za uongozi kwa
lengo la kumuandaa kuwa kiongozi bora wa sasa na hapo baadae.
“Lengo
mahususi ni kumuandaa mtoto wa kike kuwa kiongozi, tunaposema mabinti zetu
wagombee nafasi za uongozi haimaanishi wagombee Uchaguzi wa Serikali za Mitaa,
sababu umri wao ni mdogo, hawajafikia hapo bali wanachotakiwa kufanya ni
kugombea uongozi katika maeneo yao walipo. Mfano shuleni, makanisani na hata
misikitini. Sasa inahimizwa sana kwa watoto wa kike kujitokeza na kushiriki
nafasi hiyo, kwa maana hiyo tunamuandaa mtoto wa kike kuwa kiongozi bora wa
baadae mwenye kujiamini, kusimama mbele za watu, kuzungumza na kujenga hoja”
alisisitiza Matata.
Kwa
upande wake Mwalimu wa Shule ya Msingi Lukali, Mwl. Venance Kikoti, alitoa
maoni yake katika kuelekea maadhimisho wa siku ya mtoto wa kike duniani kuhusu
swala zima la uongozi “wanawake wana haki kama wanaume. Hivyo, washiriki katika
mgawanyo wa madaraka katika kugombea” alisema Mwl. Kikoti.
Nae
mwanafunzi wa Shule ya Msingi Lamaiti, Sifa Jobumuzenga, alielezea changamoto
ambazo zinawafanya washindwe kujitokeza katika kugombea nafasi za uongozi “kuna
changamoto nyingi za ukatili wa kijinsia kama ubakaji ni kikwazo kwahiyo
tunaomba serikali ikomeshe ukatili wa kijinsia kwa watoto”.
Tamasha
hilo lililoandaliwa na Msichana Initiatives lilidhaminiwa na wadau kutoka kwa
taasisi na mashirika mbalimbali ya jukwaa la msichana wakiongozwa na Flaviana
Matata Foundation, M Sema, Tae, Wote sawa, Young strong mothers’ foundation, na
grammy. Tamasha lilipambwa na burudani mbalimbali kama nyimbo, mashairi,
ngonjera na ngoma kutoka takribani shule za msingi 16 zilizopo katika tarafa ya
Mndemu na vikundi vya ngoma kutoka kwa wananchi wa tarafa hiyo.
MWISHO
Comments
Post a Comment