Jiji la Dodoma wahamasishwa kujiandikisha orodha ya wapiga kura


Na. Faraja Mbise, DODOMA

Wananchi wamehamasishwa kujitokeza kwenda kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura ifikapo Oktoba 11 hadi 20, 2024 kwa lengo la kuchagua viongozi wanaowataka katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba, 2024.




Ushauri huo ulitolewa na Diwani wa Viti Maalum Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Asma Karama muda mfupi kabla ya kuanza kikao cha Kamati ya Mipango miji na Mazingira katika Shule ya Sekondari Umonja iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Karama ambae ni Naibu Meya Mstaafu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma alitoa rai kwa wana Dodoma na wananchi wote kwa ujumla kujitokeza kushiriki katika kujiorodhesha kwenye daftari la wapiga kura kwa sababu ni muhimu kwa wananchi kutumia haki yao. Alisema kuwa kuwa uchaguzi utawasaidia kupata viongozi bora.

“Uchaguzi ni gharama, hivyo serikali hugharamia chaguzi kwa ajili ya kukupa haki wewe mtanzania, ikiwa na maana wanataka uchague kiongozi unayemtaka sio uchaguliwe kiongozi” alisema Karama.

Pia aliongeza kuwa mwananchi mwenye sifa za kujiandikisha aende akajiandikishe ili aweze kumchagua kiongozi anayemtaka na asisubiri kuchaguliwa.

Kwa upande wake Diwani wa Viti Maalumu Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Rosemary Nitwa aliwaomba wananchi wasilalamike uchaguzi ukiisha bali wajitokeze mapema katika kujiandikisha ili kuchagua viongozi wanaowataka. Aidha, aliwahamasisha wananchi wenye sifa kwenda kujiandikisha kwenye orodha ya daftari la wapiga kura.





“Sasa wananchi, nipo hapa nakuomba uende ukajiandikishe kwenye daftari kuanzia tarehe 11 hadi tarehe 20, Oktoba, 2024 kwa ajili ya kwenda kupiga kura ya kumchagua mwenyekiti wa serikali ya mtaa unayempenda na wajumbe wake watano. Ninawaomba sana sana usikae kwa kulalamika nyumbani kwamba siendi alafu baadae unalalamika kwamba hujapiga kura” alisema Nitwa.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma