Mradi wa majaribio wa usimamizi taka kuanza Dodoma

Na. Asteria Frank, DODOMA

Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira wanatekeleza mradi wa majaribio wa usimamizi wa taka za plastiki katika Jiji la Dodoma kwa lengo la kuhamasisha njia bunifu katika usimamizi wa taka za plastiki kupitia dhana ya uchumi rejeshi ili kupunguza taka za plastiki kwenye mazingira na kuboresha maisha na uchumi wa taifakwa ujumla.




Baada ya kutembelea na kukagua maendeleo ya mradi huo uliopo katika Kata ya Chamwino, Afisa Mazingira wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Aliy Mfinanga, alisema kuwa mradi wa majaribio utawanufaisha na kuwawezesha jamii na vikundi vya usafi kufanya shughuli za ukusanyaji na usafirishaji wa taka katika Kata ya Chamwino kwa nia ya kutia thamani kupitia dhana ya uchumi rejeshi ili kutunza Mazingira kutokana na plastiki.

“Tumeshazoea kuona msisitizo mkubwa kuwa taka ni taka na kwamba haifai tena, lakini kupitia mradi huu wa majaribio tunataka kuonesha jamii kuwa tunaweza kuongeza thamani ya taka kutokana na plastiki ili kuweza kufanya dhana nzima ya uchumi rejeshi” alisema Mfinanga.




Alisema kuwa wanategemea kuwa na mashine ambayo itatumika kusaga chupa za plastiki ambazo zitakuwa zimetoka mtaani, kwenye makazi, masoko, maeneo ya biashara na kwenye taasisi sehemu ambapo vikundi hivi vya Kata ya Chamwino vinafanya kazi.

“Lengo letu ni kusaga chupa za plastiki na kuzisafirisha kwenda Dar-es-Salaam kwaajili ya kutengeneza bidhaa nyingine za plastiki ikiwa ni pamoja na vyombo vya plastiki kama vifaa vya umeme, samani na kadhalika. Kwahiyo, kupitia mradi huu wa majaribio tunafanya kwenye ngazi ya vikundi na tutaufanya muda wa majaribio ili tuweze kuona namna gani tunaweza kuu ‘upscale’ kulingana na lengo tulilojiwekea”.

“Tunatarajia pia uchumi wa vikundi vinavyo fanya shughuli hii kupanda kidogo kwasababu kwa sasa wanafanyakazi ya kukusanya na kusafirisha taka. Lakini kupitia mradi huu wa majaribio wa usimamizi wa taka za plastiki wanaenda kujiongezea kipato kwasababu kilo ya chupa sasa hivi inauzwa shilingi 300 wenyewe kwakuwa wanafanya hii kazi inamaanisha watakuwa wanapata ‘material free of charge’ na baada ya kusaga tunategemea kulingana na soko la sasa ni kuanzia shilingi 800 mpaka 1,200 na mashine yetu kwa siku inaweza kusaga nusu tani ambazo ni takribani kilo 500” alisema Mfinanga.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma