Mkoa wa Dodoma kinara Mazingira ya Uwekezaji

Na. Asteria Frank, DODOMA

Mkoa wa Dodoma umeibuka kinara kwa kuwa mkoa wa kwanza kupokea tuzo za uwekezeji na utengenezaji wa mazingira wezeshaji ya biashara kutoka kwa Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Biashara, Dkt. Samia Suluhu Hassan.




Tuzo hiyo imekabidhiwa na Mwenyekiti wa “Chember of Commerce” (TCCIA) kwa Mkuu wa Mkoa Dodoma, Rosemary Senyamule katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa niaba ya Dkt. Samia Suluhu Hassan tarehe 7 Oktoba, 2024.

Senyemale alisema kuwa kupokea tuzo hiyo ni heshima kubwa sana na inahamasisha namna ya kuendelea kuboresha mazingira wezeshaji ya biashara kila siku. “Sisi kwa Mkoa wa Dododma tunajua tunazo fursa nyingi lakini pia tunao wafanyabiashara wengi kwa vitengo mbalimbali na tunashukuru kuwa tuzo hizi tunazipata sio kwa Serikali ya Mkoa kusema sisi tunafanya vizuri, Tuzo hizi zinatolewa baada ya wafanyabiashara wenyewe kusema tunaonaje huduma tunazo zipata kutoka serikalini” alisema Senyamule.

Aidha, Mwenyekiti wa TCCIA Dodoma, Vivian Komu, alitoa taarifa kuwa Mkutano wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) uliyofanyika Ikulu Dar-es-Salaam Julai 29, 2024 na Mkao wa Dodoma kuwa wa kwanza kupokea tuzo ya kuendesha mabaraza ya biashara.




Alisema kuwa tuzo hiyo ilitokana na Mwenyekiti wa Baraza la Biashara Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule. “Kwa kusimamia majukumu ya wafanyabiashara na kusikiliza kero na kuwa mstari wa mbele katika kujitoa kwenye mabaraza ya biashara na ndio maana tumeweza kupata nafasi hiyo ya kuwa mshindi wa kwanza kitaifa” alisema Komu.

Nae Katibu Mtendaji wa TCCIA Dodoma, Ringo Iringo alisema kuwa anampongeza Mkuu wa Mkoa Dodoma kwa tuzo aliyepewa na Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Biashara, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia Rosemary Senyamule kama Mkuu wa Mkoa Dodoma kwa maana amekuwa akijitoa sana kwa wafanyabiashara. “Mkoa wa Dodoma ulikuwa na changamoto nyingi sana katika maeneo ya uwekezaji upatikanaji wa viwanja kwaajili ya uwekezaji lakini maeneo mbalimbali katika sekta binafsi za mkoa wetu. Mkuu wa mkoa amekua wa haraka sana kufikika lakini pia amekuwa akichajisha na kuhamasisha kufanyika kwa baraza la biashara” alisema Iringo.

MWISHO

 

 

 

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma