Maekelezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 yatolewa Jiji la Dodoma

Na. Asteris Frank, DODOMA

Msimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko ametoa maelekezo ya uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 kwa umma.


Msimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko akitoa Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 kwa umma


Akizungumza mbele ya vyombo vya habari ofisini kwake leo tarehe 26 Septemba, 2024 kuhusu maekelezo ya uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 alisema kuwa Msimamizi wa Uchaguzi amepewa mamlaka ya kutoa maelekezo kuhusu uchaguzi. “Maelekezo haya yanatolewa siku 62 kabla ya siku ya uchaguzi, kwa lengo la kuhakikisha kuwa taratibu zote zinafuatwa na kwamba wapiga kura Pamoja na wagombea wanapata taarifa zote zinazohitajika kwa wakati. Maelekezo haya yanafafanua hatua zitakazo ongoza mchakato wa uchaguzi, kuanzia uandikishaji wa wapiga kura, uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kugombea, uteuzi wa wagombea na tarehe ya siku ya uchaguzi. Maelekezo haya yanalenga kutoa muongozo ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa uwazi, haki na usawa na kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa” alisema Dkt. Sagamiko.

Aliongeza kuwa kwa mujibu wa tangazo la uchaguzi lililotolewa kwa kuzingatia kanuni ya nne ya kanuni ya uchaguzi wa viongozi wa mamlaka za serikali za mtaa (tangazo namba 574), uchaguzi utafanyika tarehe 27 Novemba, 2024. Kwa mujibu wa kanuni ya 11 (GN. Na. 574 (Mamlaka za Miji), zoezi la uandikishaji wa wapiga kura litafanyika kuanzia tarehe 11-20 Oktoba, 2024 katika vituo vilivyopangwa, aliongeza.

Akiongelea sifa za kupiga kura kwa wakazi alisema kuwa umri kuanzia miaka 18. “Kwa mujibu wa kanuni ya 13 GN. Na. 574 wakazi wote wenye umri wa miaka 18 au zaidi na waliokidhi masharti ya kisheria wanahimizwa kushiriki katika uchaguzi huu. Kwa mujibu wa kanuni ya 17 GN. Na 574 wakazi wenye umri wa miaka 21 au zaidi wanaotaka kugombea nafasi za mwenyekiti wa mtaa, wajumbe za kamati ya mtaa, kundi mchanganyiko na kundi la wanawake wanahimizwa kuchukua fomu ya kugombea katika ofisi ya msimamizi msaidizi wa uchaguzi” alisema.

Kuhusu kuchukua na kurudisah fomu, alisema kuwa kwa mujibu wa kanuni ya 17 GN. Na. 574 fomu za kugombea zitatolewa na kutakiwa kurudishwa kuanzia tarehe 1-7 Novemba, 2024 kwa msimamizi msaidizi wa uchaguzi. “Kwa mujibu wa kanuni ya 17 GN. Na. 574 uteuzi wa wagombea utafanyika tarehe 8 Novemba, 2024” aliongeza.

MWISHO

 

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma