Gari la Darasa Tembezi latembelea Dodoma Media College

Na. Asteria Frank, DODOMA

Gari la Darasa Tembezi kutoka Halmashauri ya Jiji Dodoma limetembelea Dodoma Media College kwa lengo la kuelimisha kuhusu uandikishaji wa orodha ya wapiga kura kuelelea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.


Gari la Darasa Tembezi limewapa wanafunzi wa chuo hicho elimu ya kujiandikisha kwenye orodha wapiga kura zoezi liloanza tarehe 11 Oktoba, 2024 na kuendelea hadi tarehe 20 Oktoba, 2024 na kuwataka washiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwasababu ni haki yao na ni muhimu kuchagua viongozi wa mitaa wanayoishi.

Mwenyekiti wa uelimishaji na uhamasishaji  wa Darasa Tembezi, Shadaiya  Hassan aliwaelimisha wanafunzi kuwa kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika tarehe 27 Novemba, 2024 na kusema kuwa wanatakiwa kujiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura katika ofisi za mitaa, shule za msingi na sekondari, zahanati na vituo vya afya, maeneo ya wazi yenye mikusanyiko ya watu na majengo mengine ya taasisi za umma yaliyopo katika mitaa au vitongoji ili aweze kushiriki kuchagua mwenyeki pamoja na wajumbe wa kamati ya utekelezaji.

Alisema kuwa kuna utofauti kati ya kujiandikisha katika daftari la kudumu la mpiga kura ambalo linamfanya mwananchi kupata kadi ya kupigia kura mwaka 2025 kwenye kuchagua diwani, mbunge na raisi. Kujiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura ni kwaajili ya kupata sifa ya kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na linabeba orodha ya wananchi wanaoishi katika eneo husika.

“Zoezi la kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la mpiga kura halihusiani kabisa na Uchaguzi wa Serikaliza Mitaa. Kwahiyo, ili kupata sifa ya kushiriki Uchaguzi wa Serikari za Mitaa ni lazima ujiandikishe kwenye orodha ya wapiga kura katika mitaa tunayotoka” alisema Hassan.

Aliongeza kuwa kupata sifa ya kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni lazima uwe Raia wa Tanzania, uwe na umri wa miaka 18 na kuendelea , ni mkazi wa mtaa ambao uchaguzi unafanyika, uwe na akili timamu na awe amejiandikisha kupigakura katika mitaa husika  na zoezi la kujiandikisha  ni la mda mfupi.

Mwanafuzi wa ngazi ya Cheti wa Dodoma Media College, Martin Tulo alisema kuwa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unatuhusu watu wote tofauti na dhana aliyokuwa nayo kuwa wagombea wa uchaguzi ni watu wenye umri mkubwa na wazee kumbe na vijana tunapaswa kushiriki sio tu kupiga kura hata kugombea.

“Kama vijana kuna faida nyingi za kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ikiwa moja wapo ni kupata haki yako ya msingi, kushiriki katika vikao vya maamuzi na pia kupata uzoefu wa uongozi kwa wale wanaotaka kuja kuwa wanasiasa hapo mbeleni” alisema Tulo.

MWISHO

 

 

Comments

Popular Posts

Jiji la Dodoma lapewa angalizo lishe bora kwa wananchi

RC Dodoma apongeza wafugaji kwa ushiriki wa Paredi ya Mifugo

Rais Samia: Tumieni kikamilifu Miundombinu, Teknolojia na mitaji iliyowekezwa katika Kilimo, Uvuvi na Mifugo