Ubalozi wa Sweden kuendelea kushirikiana na Tanzania

Na. Faraja Mbise, DODOMA

Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Charlotta Macias ametembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na kufanya mazungumzo na viongozi wakuu kutoka ofisi hiyo wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule.


Katika mazungumzo hayo, Balozi Macias alisema wanashirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo Mpango wa kunusuru Kaya Masikini nchini (TASAF), elimu na katika Taasisi za kidemokrasia.

Balozi Macias aliongeza kwa kusema kuwa watashirikiana katika kutoa ujuzi na teknolojia katika maeneo mbalimbali ya uwekezaji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule aliualika Ubalozi wa Sweden kuja kuwekeza makao makuu ya nchi jijini Dodoma. Aliwaeleza fursa mbalimbali za uwekezaji ikiwemo masuala ya kilimo cha zabibu kwasababu ndio kipaumbele cha Mkoa wa Dodoma.

Ziara hiyo iliambatana na zoezi la kutembelea Mji wa Serikali Mtumba, maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya mabalozi na Ofisi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala bora.

MWISHO

 

Comments

Popular Posts

Global Affairs Canada yafurahishwa na utekelezaji wa Mradi wa AHADI katika Kata ya Chamwino

Shilingi Bilioni 7 zatekeleza miradi ya maendeleo Kata ya Miyuji

Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota