DC Dodoma akagua maendeleo ya ujenzi wa Uwanja wa Ndege Msalato

Na. Asteria Frank, DODOMA

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kishirikiana na Benki ya maendeleo ya Afrika (AFDB) inatekeleza mradi wa ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato.


Kiwanja hiko cha Ndege cha kimataifa Cha Msalato kinajegwa kwa awamu kwa kufuata mpango mkakati wa utekelezaji wa mradi huo ukiwa na lengo la kurahisisha usafiri kati ya Tanzania na nchi jirani pamoja na uboreshaji wa usafiri wa ndani.

Mkuu wa Wilaya wa Jiji la Dodoma, Alhaji Jabir Shekimweri alifanya ziara katika mradi huo ili kuangalia maendeleo ya ujenzi wa uwanja na alisema kuwa Suma JKT wanadhamana na ujenzi huo kwaajili ya ulinzi kwa kudhibiti matendo ya wizi unaofanyika.

Alisema kuwa amefarijika sana kupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi na juhudi kwenye ‘package one’ ni asilimia 75 na jitihata ya ‘package’ ya pili ni asilimia 43.6.

"Sehemu ya taarifa kulikiwa na changamoto na moja wapo ni udokozi wa kwenye mradi na tumepata nafasi ya kufanya mjadala mpana na kwa bahati na sisi tulikiwa na taarifa hizi za awali. Kwahiyo, tulihakikisha wadau wanaohusika na usalama wa eneo la mradi tunao katika ziara hii tupo na Suma JKT kwakutoa dhamana kwenye eneo hili. Mkandarasi pia anawajibika pamoja na mteja ila kila mmoja akisimama kwenye nafasi yake matukio ya udokozi hayatatokea" alisema Alhaj Shekimweri.

Aliongeza kuwa ujenzi wa uzio unaweza kutatua changamoto ya udokozi ila pia kutoa elimu ya uzalendo kwa vijana kuhusu kufahamu maana ya kushiriki kwenye miradi ya kimkakati kama hiyo na kupunguza ubora kwenye udokozi. Aliongeza kuwa ni ngumu sana mtu ambae hausiki na ujenzi huo kufahamu maeneo ambayo vifaa vya ujenzi vinahifadhiwa.

“Tunaelekea kwenye uchaguzi na kunawafanya kazi ambao ni watanzania na wanahaki ya kupiga kura na kuna watu wengi ambao wapo hapa na wengine walihama kwenye maeneo yao ya kiuchaguzi. Hivyo, inabidi wakaboreshe taarifa zao katika daftari la kudumu la mpiga kura”, alisema.

MWISHO

 

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma