Posts

Showing posts from May, 2024

Usafi wa Mazingira Kipaumbele Kata ya Chamwino

Image
Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO CLUB ya Mazingira ya Shule ya Sekondari Hijra imeshiriki zoezi la usafi wa mazingira pembezoni mwa barabara inayoelekea katika makaburi ya Hijra urefu wa takribani mita 200 kwa kufyeka majani, kuokota taka ngumu na makopo ili kuweka viunga vya barabara hiyo safi. Akitoa shukrani baada ya zoezi hilo, Afisa Mtendaji Kata ya Chamwino, Lucas Mkelege alisema kuwa uongozi wa Shule ya Sekondari Hijra umeonesha mfano mzuri kupitia Club yake ya Mazingira. “Mtakumbuka kuwa tangu kuanzishwa kwa Club ya Mazingira katika Shule ya Sekondari Hijra mwaka 2023 imekuwa mstari wa mbele katika suala ya usafi wa mazingira. Nakumbuka malengo ya club hiyo pamoja na mambo mengine ni kuwajengea wanafunzi moyo wa uzalendo na kushiriki masuala ya kijamii ikiwemo kudumisha usafi wa mazingira, asanteni sana” alishukuru Mkelege. Kata ya Chamwino imekuwa mstari wa mbele katika masuala ya usafi wa mazingira ikiwa na muitikio mkubwa wa wananchi kushiriki usafi wa pamoja wa mazingira. ...

Osterbay Dodoma wajitokeza usafi wa mazingira

Image
  Na. Dennis Gondwe, KIWANJA CHA NDEGE WANANCHI wa Mtaa wa Osterbay, Kata ya Kiwanja cha Ndege Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamejitokeza kufanya usafi wa mazingira katika eneo la Shule ya Msingi Mlimwa B kwa lengo la kuweka mazingira safi na kuepuka na magonjwa ya mlipuko kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla. Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Mtendaji Mtaa wa Osterbay, Ashura Iberia alipokuwa akiongea na wananchi wa Mtaa wa Osterbay waliojitokeza kwa wingi kufanya usafi wa mazingira katika Shule ya Msingi Mlimwa B. Iberia alisema “leo tumefanya usafi wa mazingira kuzunguka Shule ya Msingi Mlimwa B, wananchi wa Mtaa wa Osterbay wamejitokeza kwa wingi kufanya usafi wa mazingira. Lengo la kufanya usafi huo ni kuweka mazingira ya shule safi ili wanafunzi ambao ni watoto wetu wasome katika mazingira safi na salama. Lakini pia kuwaepusha wanafunzi na jamii inayozunguka shule hii na magonjwa ya mlipuko. Zoezi hili nimelisimamia mimi mwenyewe Afisa Mtendaji Mtaa wa Osterbay ili kutoa cha...