Shule ya Msingi Chinangali wapewa elimu ya Uzalendo

Na. Leah Mabalwe, CHAMWINO

Wanafunzi wa shule ya Msingi Chinangali Kata ya Chamwino wapewa elimu juu ya uzalendo wa nchi yao.



Hayo yalijili baada ya Afisa Ushilikishwaji wa Jeshi la Polisi Kata ya Chamwino, A/Insp Isiaka Shabani kutembelea shule hiyo na kutoa mafunzo ya uzalendo na kusema kuwa kila wanafunzi ni jukumu lake kuwa mzalendo.

“Kila mwanafunzi ni jukumu lake kuwa mzalendo na kuachana na matendo mabaya ambayo yanajikita katika ukatili na badala yake kuwa mzalendo katika Taifa lake kwa kumtolea mfano Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan” alisema A/Insp. Shabani.

Aidha, aliongeza kwa kuwataka wanafunzi hao kujua umuhimu wa Bendera ya Taifa maana yake hususani rangi zinazopatikana katika Bendera ya Taifa ni kielelezo kikubwa cha Taifa.

Pia alimalizia kwa kuwasihi wanafunzi  hao wa Shule ya Msingi Chinangali kuwa  inapaswa kuwa mzalendo  popote pale watakapo kuwepo na uzalendo huanzia ndani ya moyo wa mtu na kila Mtanzania ni jukumu lake kuwa mzalendo.

Nchi ya Tanzania ni nchi mojawapo kati ya nchi ambazo zinadumisha na kuendeleza uzalendo katika nchi na kila mtu ni jukumu lake kuipenda na kuidhamini nchi yake  na kuweka  maslahi ya taifa lake mbele Neno uzalendo linamaana kubwa katika nchi yetu  na nijukumu letu sote sisi kama Watanzania  kuidhamini Nchi yetu.



MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma