KISASA SEC YANUFAIKA NA UWEKEZAJI WA RAIS, DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

SHULE ya Sekondari Kisasa ni mnufaika wa uwekezaji mkubwa unaofanywa na serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika sekta ya elimu na kuchangia kuongeza kiwango cha ufaulu.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Kisasa, Mwl. Fredy Nyandoro alipokuwa akisoma taarifa ya shule


Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Shule ya Sekondari Kisasa, Mwl. Fredy Nyandoro alipokuwa akisoma taarifa ya shule hiyo katika Mahafali ya 15 ya kidato cha Nne ya shuleni hapo.

Mwl. Nyandoro alisema “ndugu mgeni rasmi, shule yetu tumekuwa na mafanikio kadhaa tangu kuanzishwa mwaka 2006. Mafanikio hayo ni kuongeza ufaulu mwaka hadi mwaka, kuongeza idadi ya watahiniwa na idadi ya vijana wanaojiunga elimu ya juu na vyuo vya kati imeongezeka. Shule imefanikiwa kuongeza miundombinu mwaka 2019 tulianza kujenga jengo la utawala na limekamilika. Mwaka 2021 tukapata mradi wa kuongeza madarasa kwa fedha za Uviko- 19 tulikuwa na madarasa matatu na kufanya madarasa kufikia 23. Tunaishukuru sana serikali yetu na mama yetu, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa ambao ameufanya katika sekta ya elimu na Shule ya Sekondari Kisasa ni mnufaika mkubwa wa uwekezaji huo”.

Mafanikio mengine aliyataja kuwa ni kupata vifaa vya kutosha vya maabara za sayansi mwaka wa fedha 2021/2022. “Mwaka 2023 tumepokea zaidi ya vitabu 2,000 vya masomo mbalimbali. Shule yetu ina maktaba bora niongoni mwa shule za sekondari nchini. Maktaba yetu imesheheni vitabu lakini pia tuna mfumo wa Tehama na pale vijana wetu wanaposoma, wanasoma kwa utulivu tuna kiyoyozi” alisema Mwl. Nyandoro kwa furaha.

Kwa upande wa mwanafunzi wa kidato cha Nne, Benedict Herman alisema kuwa amejifunza uongozi na taaluma kwa kipindi alichosoma shuleni hapo. “Nimejifunza mambo mbalimbali, nimejifunza uongozi, namna ya kuzungumza na watu, stadi za maisha na taaluma imenisaidia kuongeza uelewa na kupanua ubongo wangu. Kwa upande wa mtihani wa taifa wa kidato cha Nne, maandalizi maandalizi ni mazuri na tuliweza kufanya mitihani mbalimbali tangu kidato cha kwanza. Tumefanya mitihani ndani na nje ya shule kwa lengo la kujipa uzoefu wa jinsi mitihani inavyotungwa. Matarajio yangu ni kuendelea na elimu ya kidato cha Tano na Sita hadi chuo kikuu” alisema Herman.

Ikumbukwe kuwa Shule ya Sekondari Kisasa ilianza mwaka 2006 ikiwa na wanafunzi 20 na walimu watatu sasa ina wanafunzi 869 na walimu 55.



MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma