DODOMA ISIYO NA KERO ZA ARDHI YATAJWA

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

RAIS, Dkt. Samia Suluhu Hassan anataka wananchi wa Dodoma wafurahie makao makuu yasiyokuwa na kero wala migogoro ya Ardhi.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule (kushoto) akikabidhi moja ya Hati zilizotolewa siku a tatu ya utekelezaji wa Kliniki ya Ardhi jijini Dodoma


Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule alipokuwa akiongea na mamia ya wananchi waliojitokeza kuhudumiwa na kutatuliwa kero zao katika Kliniki ya Ardhi iliyo katika siku yake ya tatu jijini Dodoma.

Senyamule alisema “niwahakikishie Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, mama mwenye upendo na mama anayewapenda watanzania, jambo hili halitaki na anatamani wananchi wa Dodoma wafurahie makao makuu ya Dodoma na watafurahia kama watapa haki zao. Ndiyo maana amekuwa akituagiza kutatua kero zao hasa za Ardhi katika Jiji la Dodoma. Kama mkoa baada ya kupokea maelekezo ya Mheshimiwa Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi wametuagiza kuhakikisha tunamaliza kero za Ardhi kwa wananchi wa Dodoma”.

Alisema kuwa mkoa umetengeneza mpango mkakati wa mwaka mmoja kuhakikisha kero za Dodoma zinaisha. “Kuanzia mwezi Julai hadi Desemba, 2023 kuna kero kubwa zinazogusa makundi makubwa tunaendelea kuzitatua. Kuanzia mwezi Januari hadi Juni, 2024 tunamalizia kero za mtu mmoja mmoja ambazo hazikukamilika kwa wakati. Nimpongeze Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mkurugenzi wa Jiji na Katibu Tawala Mkoa baada ya mkakati huu wameendelea kuunyumbulisha ili ukamilike vizuru wameongeza na ubunifu. Mfano kuanzisha hii Kliniki ya Ardhi ni moja ya mkakati wa kukamilisha kero kwa wakati” alisema Senyamule.

Akimkaribisha Mkuu wa Mkoa kuzungumza na wananchi, Mkuu wa wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alisema kuwa timu ya wataalam imejipanga vizuri. “Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa tupo hapa tangu kutekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Rais, tusikae ofisini, tutoke kuwasikiliza wananchi na kero ya Ardhi kwenye jiji letu ni kubwa. Kutokana na ukubwa wake Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa ulituongoza vizuri tukaandaa mkakati wa kushughulikia kero ya Ardhi. Mkakati mmoja wapo ni kuwa na kliniki za Ardhi, ambayo imeanzia hapa halmashauri na itakuwa ikihama kwenda maeneo ya kata kuwasilikiza wananchi” alisema Alhaj Shekimweri.

Katika hafla hiyo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma alikabidhi Hati kwa wananchi 15 katika siku ya tatu ya utekelezaji wa Kliniki ya Ardhi jijini Dodoma.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma