BARAZA LA MADIWANI JIJI LA DODOMA LAMSHUKURU RAIS SSH
Na.
Dennis Gondwe, DODOMA
BARAZA
la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma linamshukuru Rais, Dkt. Samia
Suluhu Hassan kwa miradi mingi ya maendeleo inayotekelezwa katika jiji hilo kwa
kusimamia ubora na thamani ya fedha.
![]() |
Mwenyekiti wa Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe akimshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan |
Kauli
hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya
Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe katika mkutano wa baraza hilo wa
kuwasilisha taarifa za maendeleo kutoka kwenye kata uliofanyika katika ukumbi
wa mikutano wa halmashauri ya jiji hilo.
Prof.
Mwamfupe ambae ni Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema kuwa
halmashauri yake inaweka msisitizo katika kupitia utekelezaji wa miradi ya
maendeleo. “Sisi Jiji la Dodoma tunawiwa kumshukuru Mheshimiwa Rais, kwa sababu
ni wanufaika wakubwa wa miradi inayotoka serikali kuu. Shukrani zetu kubwa
zaidi ni usimamizi wa miradi, kuhakikisha fedha zinatumika ipasavyo. Mahitaji ya
nchi ni makubwa sana, mahitaji ya Dodoma kama mkoa, mahitaji ya Dodoma kama
halmashauri ni makubwa sana lakini sisi kwa hadhi yetu kama Halmashauri ya Jiji
la Dodoma ambalo ni makao makuu ya nchi tunajikuta tumepewa uzito mkubwa sana. Namna
pekee ya kumshukuru Mheshimiwa Rais ni kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo”
alisema Prof. Mwamfupe.
Akiongelea
mambo ya kuzingatia katika utekelezaji wa miradi hiyo alisema kuwa ni kujikita
katika ubora na matumizi ya fedha. “Katika utekelezaji wa miradi hii mambo
makubwa mawili yanazingatiwa. Matumizi sahihi ya rasilimali fedha na jambo la
pili ambalo linaoana kabisa na jambo la kwanza ni ubora wa miradi yetu
tunayoitekeleza. Haisaidii kuwa na matumizi sahihi ilimradi vitabu vime ‘balance’,
lazima ‘balance’ nyingine itokane kwenye thamani ya mradi, kuhakikisha kweli
miradi imekuwa ya kiwango cha juu kinachotegemewa” alisisitiza Prof. Mwamfupe.
Aidha,
alisema kuwa halmashauri yake haitasita kuchukua hatua kwa uzembe utakaofanyika
katika kusimamia utekelezaji wa miradi. “Hatutasita kufika mahali kuona kama
hakuna dalili nzuri ya thamani ya mradi huo, tutachukuliana hatua ili
kuhakikisha tunatumia fedha vizuri kama ilivyopangwa” aliongeza.
Katika
hatua nyingine, Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma
lilishuhudia Diwani, Julius Chimombo akila kiapo cha udiwani kufuatia kushinda
katika uchanguzi mdogo wa udiwani uliofanyika katika kata ya Nala hivi
karibuni.
MWISHO
Comments
Post a Comment