Halmashauri ya Jiji la Dodoma yashiriki maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma

Na. Nancy Kivuyo, DODOMA

Halmashauri ya Jiji la Dodoma inashiriki maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma, yanayojumuisha Taasisi za Serikali, Bunge na Mahakama, katika uwanja wa Chinangali Park jijini Dodoma.



Maadhimisho hayo yanalenga kuonesha uwajibikaji wa taasisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi pamoja na kutoa elimu mbalimbali.

Hayo yalisemwa na Afisa Utumishi, Patrick Bashemela alipokuwa akitoa utambulisho wa huduma zinazopatikana katika banda la halmashauri. “Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanatupa fursa nzuri ya kuonesha namna huduma zetu zinawafikia wananchi, banda letu linatoa huduma ya ukataji wa leseni ya biashara, elimu ya matumizi ya mfumo wa Tausi, elimu ya juu ya mikopo ya asilimia 10 na huduma ya uuzaji viwanja. Huduma zote muhimu zinazotolewa halmashauri, zitapatikana hapa kwa siku zote za maadhimisho” alisema Bashemela.

Alimalizia kwa kuwakaribisha watumishi wote na wananchi kutembelea banda la halmashauri ili kupata elimu ya huduma mbalimbali na pia kupata huduma wanazohitaji. “Napenda kuwakaribisha wote katika uwanja wa Chinangali Park hasa katika banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma, tunatoa huduma zote muhimu. Karibuni sana” alimaliza Bashemela.




Maonesho hayo yatafanyika kwa muda wa siku nane na yanatarajiwa kutoa fursa ya watumishi kujifunza mambo mbalimbali na kupata huduma zilizosogezwa karibu kutoka katika mabanda tofautitofauti. Kaulimbiu ya maadhimisho hayo inasema “Himiza matumizi ya mifumo ya kidijiti ili kuongeza upatikanaji wa taarifa na kuchagiza uwajibikaji”.

MWISHO

 

Comments

Popular Posts

Jiji la Dodoma lapewa angalizo lishe bora kwa wananchi

RC Dodoma apongeza wafugaji kwa ushiriki wa Paredi ya Mifugo

Vijana waalikwa kushiriki Kongamano S/M Mbwanga