Wazazi washauriwa kununua vifaa vya shule kwa bei elekezi

Na. Aisha Ibrahim, DODOMA                                                                                                                                                                                  Wafanyabiashara  wanaojihusisha na kuuza vifaa  vya shule kwa wanafunzi, wanaopatikana  Mtaa wa One Way, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, wamewaasa  wazazi na walezi  kujitokeza kununua vifaa hivyo kwa bei elekezi bila kuhofia, kwasababu mpaka sasa bei ni ya kawaida kama ilivyokuwa miezi iliyopita .

Hayo yalisemwa na baadhi ya wafanyabiashara wakieleza kuwa, bei ya vifaa vya shule kwa wanafunzi haijapanda kama walivyozoea misimu iliyopita hivyo, wazazi au walezi wajitokeze kwa wingi kununua vifaa vya shule kwa ajili ya watoto wao.

Noely Chibarabara alisema “bei zetu kwakweli hazijapanda, ziko palepale na hakuna shida yoyote ambayo imeweza kutokea kwamba tumepandisha bei, bei ipo palepale na bei zetu ni nzuri".

Akizungumzia kuhusu changamoto ya uzalishaji bidhaa viwandani kutokana na uhitaji mkubwa wa wateja, mfanyabiashara Paskali Faustine alisema bei inapanda msimu huu kutokana na uhitaji mkubwa wa bidhaa zitumikazo shuleni.

“Bei inapanda miezi hii kwa sababu ya uzalishaji viwandani unakuta ni changamoto, wanaotaka mahitaji ni wengi sana kwa sababu ni kipindi cha shule asilimia kubwa bidhaa zinakuwa ziko juu” alisema Faustine.

Akiongelea wafanyabiashara wanaopandisha bei katika msimu wa kuelekea shule kufunguliwa, mfanyabiashara Tonni Jamen aliwashauri kutokupandisha bei vifaa vya shule. Aidha, aliwashauri kuuza vifaa hivyo kwa bei elekezi ili kuwawezesha wazazi na walezi kumudu gharama na kuwashauri wasiogope kujitokeza kuwanunulia vifaa vya shule watoto wao ili waweze kwenda shule bila vikwazo.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma