Mila na Desturi kandamizi mwiba kwa mtoto wa kike

Na. Faraja Mbise, DODOMA

Tanzania inaungana na mataifa mengine katika kupambana na changamoto ya mila na desturi kandamizi ambazo ni kikwazo kwa mtoto wa kike katika kutimiza ndoto zake hasa katika suala la uongozi.




Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa kike Duniani yaliyofanywa na Shirika la Msichana Initiaves, jijini Dodoma, Balozi. Liberata Mulamula alisema kuwa am tot desturi kandamizi ni kikwazo kwa binti katika kuzifikia ndoto zake hasa katika uongozi.

Balozi Mulamula alisema “mila na desturi kandamizi zinamyima mtoto wa kike haki yake ya msingi ya kwenda shule kusoma. Kwahiyo, zinapunguza idadi ya wanawake kuwa viongozi. Mila na desturi kandamizi ndani ya jamii zinampa mtoto wa kike machaguzi machache ambayo yanapelekea kupoteza watoto wa kike wengi sana”.

Aidha, alisisitiza mtoto wa kike kutumia teknolojia kwa lengo la kujifunza na kuelimika hasa katika mitandao ya kijamii. Aliwataka waitumie waitumie kwa ufasaha katika kupata elimu na kuwataka kujitambua na kujiamini katika maisha akisema kuwa ndio msingi mkuu wa kuwa kiongozi bora.

“Uzuri wa teknolojia au intaneti haichagui jinsi, haina ubaguzi wa kijinsia, ni jinsi gani unaitumia kwa manufaa yako, kuongeza ujuzi wako, katika kuleta ustawi wa jamii na maendeleo ya taifa letu” alisistiza Balozi Mulamula.

Kwa upande wake Meneja miradi wa Shirika la Msichana Initiatives, Furahini Michael alizungumzia changamoto nyingi zinazomkwamisha msichana kushiriki katika kufanya maamuzi na kutaja mila na desturi kandamizi kuwa ni kikwazo kikubwa sana.

“Mila na desturi kandamizi ambazo kwa namna moja zinawatoa wasichana kwenye kushiriki nafasi mbalimbali katika kufanya maamuzi. Mfano katika ngazi ya familia, mtoto wa kike anakuwa msikilizaji na mtekelezaji tu. Kwahiyo, kutokana na hizo mila na desturi kandamizi wasichana wameachwa nyuma kwenye masuala ya uongozi” alisisitiza Furahini.

Hata hivyo, baadhi ya wadau mbalimbali wa haki za mtoto wa kike wametoa ushauri kuwa, watoto wa kike watumie teknolojia kwa matumizi sahihi na waishi maisha yao na sio kufuata maisha ya mitandaoni ambayo yatawapelekea kuua ndoto zao.

Meneja wa miradi katika Shirika la Plan International, Peter Mwakabwale alisema “kumekuwa na matumizi mabaya ya kimitandao ambayo imepelekea kuweza kuwepo na unyanyasaji kwa njia ya teknolojia, wasichana wamekuwa wakijihusisha katika mitandao kwa lengo ambalo si rafiki”.

Katika maadhimisho hayo ya siku ya mtoto duniani wadau hao walipata fursa ya kuongea na watoto wa kike kuhusiana na masuala mbalimnbali yanayohusu teknolojia na kwa namna gani wataweza kuitumia ili kufikia malengo yao na kuwasisitika kushiriki katika nafasi za uongozi pindi wawapo shuleni na katika masuala ya kijamii.

Kila mwaka tarehe 11 Oktoba, Tanzania inaungana na mataifa mengine ulimwenguni katika kuadhimisha siku ya mtoto wa kike duniani ambapo kaulimbiu kwa kwa mwaka huu 2024 ni “Msichana na Uongozi, Tumshirikishe Wakati ni Sasa”.

 MWISHO

 


Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma