JIJI LA DODOMA LAPEWA HADHI YA MKOA WA ARDHI

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WIZARA ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi yaipa Halmashauri ya Jiji la Dodoma hadhi ya kuwa Mkoa wa Ardhi kwa lengo la kuboresha huduma kwa wananchi.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Slaa


Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Slaa alipokuwa akiongea na waandishi wa habari leo katika Ofisi ya Ardhi Mkoa wa Dodoma kuhusu utekelezaji wa maelekezo ya serikali kuhusu kuboresha huduma za sekta ya Ardhi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Mwanza.

Slaa alisema “Wizara imeifanya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuwa Mkoa wa Ardhi kiutendaji ikiwa na Kamishna wa Ardhi Msaidizi ambae atahudumia eneo hilo na halmashauri nyingine kuwa na Kamishna wa Ardhi Msaidizi mwingine”.

Waziri huyo alisema kuwa wizara imeandaa utaratibu wa kutoa huduma kwa pamoja katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma utaratibu ambao utasimamiwa na wizara kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuanzia tarehe 30 Oktoba, 2023. “Hatua hizi zinalenga kuboresha utoaji wa huduma za sekta ya ardhi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Nitoe wito kwa wananchi kutumia fursa hiyo kupata huduma za sekta ya Ardhi zikiwemo upatikanaji wa hati milki, malipo ya kodi ya pango la Ardhi, utatuzi wa migogoro na utoaji wa elimu kwa wananchi” alisema Slaa.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma