Chupa 41 za damu zakusanywa Nyerere Square, wananchi wahimizwa kuendelea kuchangia
Na. Nancy Rogers, DODOMA
Jumla ya chupa 41 za damu zilikusanywa kutoka kwa
wachangiaji waliojitokeza kwa hiari katika siku ya kwanza ya Kliniki ya Upimaji
Magonjwa yasiyoambukiza
inayoendelea katika bustani ya mapumziko Nyerere Square jijin
Dodoma.
Hayo yalielezwa na Mkuu wa Timu za
Ukusanyaji Damu Kanda ya Kati kutoka Wizara ya Afya, Dkt. Leah
Kitundya ambae
alisema kuwa lengo la kampeni hiyo ni kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu
umuhimu wa kuchangia damu mara kwa mara, kwasababu mahitaji ya damu katika
hospitali yanaongezeka kila siku. “Tunaendelea kuhimiza jamii kuchangia damu
kwa hiari, kwa kuwa damu ni uhai na inaweza kuokoa maisha ya mama wajawazito,
wagonjwa wa upasuaji na wa ajali” alisema.
Mmoja wa wachangiaji damu na Mkazi
wa Miyuji, Rehema
Juma
alisema kuwa uchangiaji damu ni tendo la huruma linalookoa maisha. “Mimi
niliwahi kuongezewa damu baada ya kujifungua kwa shida, na leo niko hai kwa
sababu ya watu waliotoa damu kwa hiari. Kwa maana hiyo nawahimiza wananchi
wenzangu kusogea hapa kuchangia damu ili tuwasaidie wengine” alisema.
Nae, Mkazi wa Makole, Emmanuel Mushi ambaye alihudhuria
kliniki hiyo, alisema kuwa upimaji wa bure na elimu inayotolewa imewasaidia
wengi kuelewa umuhimu wa kuangalia afya zao. “Nilipimwa shinikizo la damu na
nimepata ushauri mzuri wa kitabibu. Ni huduma ya muhimu sana kwa jamii, japo
sijachangia damu lakini wakati ujao nitachangia ili kugusa maisha ya wengine”
alisema.
MWISHO
Comments
Post a Comment