Bima ya Taifa ya Afya yatoa huduma kieletroniki
Na. Leah Mabalwe, DODOMA
Maboresho
ya huduma ya Bima ya Afya yamefanywa kwa kuzingatia ukuaji wa teknolojia ambapo
wananchi wanaweza kujisajili kupata huduma za bima kupitia simu zao na vifaa
vya kieletroniki vyenye ‘Internet’.
Hayo yalisemwa na Afisa Wanachama Mwandamizi, Bima ya Afya Mkoa wa Dodoma, Bakary Hamdun katika Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri wakati akiwasilisha sheria ya afya na kanuni zake.
Alisema
kuwa kila mwanachama anaetarajia kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)
anaweza kujihudumia kupitia simu ya mkononi “Mwanachama yeyote awe mtumishi au
mwananchi wa kawaida anaweza kujisajili kupitia simu yake ya mkononi. Na
anaweza kufanya hivyo bila kuwa na changamoto ya aina yoyote kwasababu huduma
hii ni rahisi pia inafanyika kwa muda mfupi” alisema Hamdun.
Kwa
upande wake Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe aliipongeza
serikali kwa hatua kubwa ya uboreshaji wa huduma ya Bima ya Afya kwa kutumia
vifaa vya kisasa vya kieletroniki.
Alisema kuwa uborehaji huo wa huduma ya bima kupitia simu janja ni rahisi, pia inaweza kuwafikia watu walio mbali na vituo vya utoaji huduma. “Nipende kuipongeza serikali kwa kufikia hatua hii ya uboreshaji wa kieletroniki kwasababu huduma hii ya Bima ya Afya itasaidia kwa watu waliopo wilaya tofauti tofauti kwa kutumia simu zao za mkononi. Pia suala hili la ukataji wa bima ni muhimu na tulitilie maanani” alisema Prof. Mwamfupe.
Nae
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaji Jabir Shekimweri aliwataka wananchi wote
kukata Bima za Afya kwasababu taasisi za afya zimekuja na njia rahisi za huduma
hiyo.
Aliongeza kwa kuwataka wamiliki wa vyombo vya moto, biashara na majengo kukatia bima ya mali zao ili kuepuka hasara pale ambapo majanga yatakapo kumba mali zao kama ajali ya moto. “Nipende kuwahamasisha wananchi muweze kukata bima hizi kwasabu zinasaidia hata pale unapopatwa na matatizo mfano ajari za barabarani au kuunguliwa na nyumba basi bima uliyoikata itakusaidia iwe hospitali na sehemu yoyote ile ambapo umempata tatizo” alisema Shekimweri.
MWISHO
Comments
Post a Comment