Global Affairs Canada yafurahishwa na utekelezaji wa Mradi wa AHADI katika Kata ya Chamwino

 

Kata ya Chamwino, imepokea ugeni kutoka Global Affairs Canada ukiongozwa na Mary Harasym aliyeambatana na Zahra Popatia ambao ni wafadhili wa mradi wa AHADI na kueleza kuridhishwa na utekelezaji wa mradi huo.




Lengo la ziara hiyo ni kufanya tathimini na kujionea kwa macho namna mradi unavyotekelezwa hususan utoaji wa elimu kuhusu maswala ya Afya ya uzazi kwa vijana wa Kata ya Chamwino.

Kwa upande ‘Promoter’ wa mradi, Khadija Ally alitoa maelezo ya kina kuhusu shughuli zinazofanyika na mafanikio yaliyopatikana kwa vijana kushiriki kwenye mafunzo yenye lengo la kuwajengea uwezo wa kufanya maamuzi sahihi kuhusu maswala Afya ya uzazi, kujikinga dhidi ya mimba zisizotarajiwa na kuwa na mipango bora ya maisha ya baadae pamoja na kuwajengea uwezo wa kuwa na shughuli za kuingiza kipato.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Chamwino, kwa niaba ya Diwani aliwashukuru wageni hao kwa kuitembelea Kata ya Chamwino na kusema kuwa mradi wa AHADI ni kielelezo kizuri cha ushirikiano baina ya kata yake na Canada.

Mradi wa AHADI unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya shirika la World Vision na TAHEA.






MWISHO

Comments

Popular Posts

Jiji la Dodoma lapewa angalizo lishe bora kwa wananchi

Rais Samia: Tumieni kikamilifu Miundombinu, Teknolojia na mitaji iliyowekezwa katika Kilimo, Uvuvi na Mifugo

IAA Tawi la Dodoma kuendelea kulea wataalam kwa vitendo