Kata ya Makole yang’ara miaka minne ya Samia

Na. Emanuel Charles, MAKOLE

 

Diwani wa Kata ya Makole, Omary Omary, aishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha miundombinu ya maendeleo kwenye sekta mbalimbali ikiwemo elimu, afya, ujenzi wa barabara na ofisi ya wafanyabiashara wadogo katika kata yake.

 



Akizungumza katika ziara ya waandishi wa habari waliotembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa kuanzia mwaka 2020 hadi sasa katika Kata ya Makole, Diwani Omary alisema kuwa anaishukuru serikali kwa kuijali Kata ya Makole kuwaboreshea miundombinu muhimu. “Kipekee nimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa miaka hii minne ambapo yupo madarakani, maboresho ambayo ametufanyia hususani sisi wana Makole kwa kutuletea miundombinu sahihi ni makubwa sana. Mheshimiwa Rais, ameboresha sekta ya elimu kwa kujenga shule ya jengo la ghorofa lenye madarasa nane na ofisi mbili za waalimu katika Shule ya Msingi Makole. Katika sekta ya afya, Zahanati ya Makole sasa wananchi wote wa kata yetu wanapata huduma ya afya nzuri na kwa usahihi, kuna hadi huduma ya ‘ultra sound’ hay ani mapinduzi makubwa. Tulitoa eneo kwa maelekezo kwaajili ya ujenzi wa Ofisi ya Machinga Mkoa wa Dodoma na sasa imekamilika na inafanya kazi” alisema Omary.



“Maboresho yote haya yana faida kubwa sana. Kwa mfano katika Shule ya Msingi Makole, utoro umepungua sana, watoto wanahudhuria masomo kwakuwa wanakaa kwa nafasi sasa. Kwa upande wa afya, huduma zimeboreka, vifaa tiba vipo na huduma ni nzuri” alisema Omar.

Nae, Katibu wa Machinga Mkoa wa Dodoma, Victor Michael aliipongeza serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa ameweza kutimiza ahadi aliyowaahidi kwa kuwajengea ofisi ya wafanyabiashara wadowadogo (Machinga) ili kuweza kutatua migogoro yao kama wafanyabiashara. “Rais wetu amekuwa akitusapoti sana sisi wafanyabiashara wa Mkoa wa Dodoma, tulimuomba kujengewa ofisi kila mkoa kwaajili ya kushughulikia matatizo yetu na bila kusita alitoa fedha kiasi cha milioni 10 na sasa tunafuraha kupata ofisi hii. Kwakweli, tunafuraha kubwa sana, sasa tunafanya kazi zetu kwa uhuru na kwa kufuata utaratibu” alisema Michael.  



Katika hatua nyingine, Shule ya Sekondari Dodoma nayo imefanyiwa maboresho makubwa kwa kuongezewa vyumba vya madarasa, vitabu pamoja na kompyuta kwaajili ya kuongeza ufanisi na ujifunzaji kwa wanafunzi. Mwanafunzi wa kidato cha Sita, Joan Kilangi aliishukuru serikali kwa kuwaboreshea miundombinu ya kujisomea. “Sisi kama wanafunzi sasa hivi tunasoma vizuri kutokana na ongezeko la madarasa kwasababu hapo zamani tulikuwa tunakaa wengi katika chumba kimoja. Kwa sasa hatukai tena kwa kusongamana. Kwa namna ya kipekee, nipende kumshuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutujengea madarasa haya, Mungu ambariki sana” alimalizia Kilangi.

 

MWISHO

Comments

Popular Posts

Mbunge Mavunde akabidhi Kompyuta kwa Kata 41 za Jiji la Dodoma

Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Majengo Dodoma watarajia makubwa Mradi wa TACTIC

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma