Dodoma Jiji U20 yatuma salamu Ligi ya Vijana
Na Mussa Richard, DODOMA
Klabu
ya Soka ya Dodoma Jiji chini ya umri wa miaka 20 imetuma salamu kwa timu
zinazoshiriki ligi ya vijana ya NBC chini ya miaka 20 baada ya kuibuka na
ushindi wa mabao 6-0 dhidi ya Tabota United chini ya miaka 20 mchezo uliochezwa
katika uwanja wa Jamhuri Dodoma hapo jana.
Akizungumza
baada ya mchezo huo Kocha mkuu wa timu hiyo, Chido Jeremiah alisema “tunamshukuru
Mwenyezi Mungu mchezo umeisha salama na tumepata ushindi wa magoli mengi na
ushindi wa kutuheshimisha na kutuweka mbele zaidi na wanaotufuata. Japo hatukua
na mchezo mzuri kipindi cha kwanza lakini wakati wa mapumziko tukawapa vijana
maelekezo ya kufanya kutokana na mapungufu tuliyoyaona kwa wapinzani wetu ndiyo
maana tuliporudi kipindi cha pili tukafanikiwa kupata mabao manne. Kwa upande
wa timu imeendelea kuimarika na vijana wameanza kujituma na niwashukuru
mashabiki wamejitokeza kuiangalia timu yao na wameona jinsi inavyocheza. Kwahiyo,
niwaombe wanadodoma wasiiache timu hii timu ni yao na waendelee kuiunga mkono
ili iweze kufanya vizuri zaidi” alisema Jeremiah.
Kwa
upande wake Bakari Mondwe ambaye ni nahodha wa timu hiyo baada ya mchezo
kumalizika alisema “mchezo umeisha, tumepata alama tatu ambazo zimetufanya
tuendelee kuwa kileleni kwenye kundi. Malengo yetu katika huu mzunguko wa pili
ni kuhakikisha tunamaliza vinara katika kundi na tunavuka katika hii hatua
kuingia katika hatua inayofuata na niwaombe mashabiki waendelee kuja kwa wingi
kwenye kila mchezo tunaocheza na sisi kama wachezaji jukumu letu ni
kuwafurahisha kwa kushinda kila mchezo ulio mbele yetu” alisema Mondwe.
Baada
ya ushindi huo Dodoma Jiji U20 ijikita kileleni katika kundi A ikiwa na Alama
16 baada ya kushuka dimbani katika michezo saba ikishinda michezo mita ikitoa
sale mchezo mmoja na ikipoteza mchezo mmoja, ikifunga mabao 15 ikifungwa mabao matano
pekee ikiwa mbele kwa alama tatu dhidi ya wapinzani wao wanaofuatia ambao ni
Azam U20 wenye alama 13. Mchezo unaofuata Dodoma Jiji U20 itashuka dimbani
Januari, 22 kuikabiri Mashujaa U20 katika uwanja wa Jamhuri Dodoma ikiwa ni
muendelezo wa mbilinge mbilinge za duru ya pili ya Ligi ya Vijana ya NBC
Tanzania Bara.
MWISHO
Comments
Post a Comment