Kata ya Ng’hong’onha mwenyeji Siku 16 za Kupinga Ukatili

Na. Mwandishi wetu, Ng’hong’onha

Kata ya Ng’hong’onha mwenyeji wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ngazi ya halmashauri yakilenga kutoa elimu na hamasa kwa jamii dhidi ya kupambana na ukatili katika jamii kuelekea miaka 30 ya Beijing.




Katika maadhimisho hayo elimu dhidi ya ukatili wa kijinsia itatolewa pamoja na kufafanua aina za ukatili wa kijinsia, taarifa za vitendo vya ukatili wa kijinsia na kuwajengea uelewa wanafunzi na watoto kuripoti taarifa za ukatili wa kijinsia katika jamii. Maeneo mengine yatakayopewa kipaumbele ni umuhimu wa kuwainua wanawake kiuchumi kama njia moja wapo ya kupambana na ukatili wa kijinsia.

Maadhimisho hayo yanayoongozwa na kaulimbiu isemayo “Kuelekea miaka 30 ya Beijing: Chagua kutokomeza ukatili wa kijinsia” yanapambwa na burudani mbalimbali kama maigizo na ngoma, mgeni rasmi ni Joseph Chotero, Mkurugenzi wa SABUDA Foundation yakifanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Ng’hong’onha.

MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma