Mbunge Mavunde kuwekeza zaidi sektan ya Elimu Dodoma
Na.
Dennis Gondwe
Mbunge
wa Jimbo la Dodoma mjini, Anthony Mavunde ameahidi kuendelea kuwekeza katika
sekta ya elimu ili kuwawezesha wanafunzi wa Dodoma kusoma vizuri na kufikia
malengo yao.
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri akitoa salamu za Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini |
Kauli
hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alipokuwa
akitoa salamu za Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini katika mkutano wa wadau wa
elimu Wilaya ya Dodoma uliofanyika katika ukumbi wa Shule ya St. Gasper jijini
Dodoma.
Alhaj
Shekimweri alisema “Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini anasema kuwa nitaendelea
kuwekeza zaidi kwenye elimu ili kuwasaidia watoto wa Dodoma kufikia malengo
yao. Nitashirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo ili kuinua na kuboresha elimu
katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma hasa katika miundombinu na mazingira
rafiki ya kusomea”.
Akiongelea
mapinduzi katika teknolojia, alisema kuwa Dodoma inaelekea kupiga mapinduzi
makubwa kwenye elimu. “Dunia inakwenda kwenye mapinduzi makubwa ya teknolojia,
lazima tutumie maendeleo hayo katika kurahisisha ufundishaji wa wanafunzi. Ni
jambo la msingi sana. Ukifika pale shule ya sekondari Dodoma utaona serikali ya
awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Ofisi ya
Rais, Tamisemi na Taasisi ya Elimu Kibaha na wafadhili imewekeza mfumo wa ‘e-learning’
na Shule ya Sekondari Dodoma ni miongomi mwa shule 10 zinazofanyiwa majaribio.
Mwalimu akiwa Kibaha mkoani Pwani au Dodoma anaweza kuwa darasani kufundisha wanafunzi
wa darasa lake, wanamuona na kufundisha wanafunzi wa shule nyingine na kumuona
na kuuliza maswali na kujibiwa” alisisitiza Alhaj Shekimweri.
Awali Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alisema kuwa kila mdau wa elimu ana nafasi katika mafanikio ya sekta ya elimu.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo akielezea lengo la mkutano huo |
“Sote tupo
hapa na tunahusika moja kwa moja kuhakikisha watoto wetu wanapata elimu bora.
Hivyo, tutajadili tulipo na jinsi ya kuendelea mbele na namna ya kutatua
changamoto za elimu. Tunajua serikali ya awamu ya sita imefanya mambo makubwa
na kuweka msingi utakaowasaidia watoto wetu na taifa letu kusonga mbele katika
maendeleo na kuboresha huduma za kijamii. Katika kuunga mkono juhudi hizo, leo
tutatoa tuzo kwa walimu waliofanya vizuri katika shule na majukumu yao, lakini
pia wapo wanafunzi ambao wamefanya vizuri katika masomo yao. Hiyo itakuwa
chachu kwa wengine kufanya vizuri zaidi.
MWISHO
Comments
Post a Comment