Mahakama zashauriwa kuyapa uzito mashauri ya kibiashara

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

MAHAKAMA nchini zimeshauriwa kutoa umuhimu kwa mashauri ya kibiashara ili yaweze kumalizika mapema na kuwawezesha wananchi kufanya shughuli za kuzalisha mali.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia katika maadhimisho ya Siku ya Sheria 



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia katika maadhimisho ya Siku ya Sheria 


Kauli hiyo ilitolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika katika bustani ya Chinangali jijini Dodoma.

Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan alisema kuwa Mahakama nchini ziharakishe kusilimiza mashauri ya kibiashara. “Tunapovutia mitaji na uwekezaji nchini na kufungua fursa za kibiashara, tunatambua uwekezaji kuambatana na masuala ya kisheria na migogoro ya kibiashara. Ni vema kwa Mahakama zetu kutoa umuhimu kwa mashauri ya aina hiyo pia” alisema Dkt. Hassan.

Aidha, alimpongeza Jaji Mkuu wa Tanzania kwa kuboresha utendaji katika Mahakama nchini. “Mheshimiwa Jaji Mkuu nataka nikupongeze wewe na Mahakama kwamba hatua nyingi mlizochukua zimekwenda kupunguza mambo mengi. Ucheleweshaji wa kesi umepungua kwa kiasi fulani na kupunguza muda wa kesi kusikilizwa kwa muda mrefu mahakamani” alisema.

Akiongelea maendeleo ya kiuchumi na haki alisema kuwa vinauhusiano wa moja kwa moja. “Mheshimiwa Jaji Mkuu, upo uhusiano mkubwa baina ya haki na maendeleo ya kiuchumi. Tunapoendelea kuvutia mitaji nchini na kuendelea kuvutia fursa za wawekezaji, ni lazima tuishi na kuzungumza ludha ya kibiashara na uwekezaji. Muwekezaji anathamini sana muda kwa sababu muda ni mali. Na hapa namaanisha muwekezaji wa ndani na yule wa nje. Ndiyo maana ni lazima mitazamo ya wadau wa Mahakama nchini ijielekeze kwenye kupunguza muda unaotumika kwenye mashauri ili wananchi watumie zaidi muda wao kwenye masuala ya uzalishaji.


Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma  akikagua gwaride maalum



MWISHO

Comments

Popular Posts

Wananchi Makutupora wafunguka changamoto ya Maji, Umeme na Shule kwa Mkuu wa Mkoa

Waziri Mchengerwa apongeza usimamizi wa miradi jijini Dodoma

Mkataba ujenzi Uwanja wa Mpira wa Miguu wasainiwa Dodoma