SERIKALI YAANZISHA KLINIKI YA ARDHI DODOMA KUTATUA KERO ZA WANANCHI
Na.
Dennis Gondwe, DODOMA
SERIKALI
imeanzisha kliniki maalum ya Ardhi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa
lengo la kusikiliza na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi ikiwa ni
utekelezaji wa maelekezo ya serikali ya awamu ya sita.
Kauli
hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Ally Gugu alipotembelea siku ya
kwanza ya utekelezaji wa majukumu ya kliniki hiyo na kuongea na mamia ya
wananchi waliojitokeza katika eneo la iliyokuwa Halmashauri ya Manispaa ya
zamani jijini hapa.
Gugu
alisema “hii ni kliniki maalum ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma akishirikiana
na Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Dodoma na Katibu Tawala Msaidizi anayehusika
na Miundombinu akiiwakilisha Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma. Lengo ni kuwasikiliza
na kutambua kero zenu kwenye masuala ya Ardhi katika Jiji la Dodoma. Tumekuja kuwasilikiza
tutambue kero zenu na wananchi wanaotaka kuhakiki maeneo yao na hati miliki
tuweze kuwapatia”.
Alisema
kuwa kliniki hiyo inaashiria dhamira ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa
na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Wizara ya Ardhi na Mkoa wa Dodoma katika
kuwahudumia wananchi. “Ndani ya wiki moja tutahakikisha tumetatua changamoto
zenu kama tutaona baada ya kujitathmini kama kuna haja ya kuendelea na zoezi
hili litakuwa endelevu. Kwa wingi huu wa wananchi tumeona tuwe na eneo kubwa
ili tuweze kuwashughulikia kwa wingi. Sisi tuwashukuru sana kwa uvumilivu na
kujitokeza kwenu mmekuwa mkishughulikiwa kwa utulivu. Tunaomba uvumilivu wenu
uendelee na sisi kama watumishi wa umma ambao Mheshimiwa Rais ametuelekeza tupo
tayari kuwasilikiza na kuwahudumia” alisema Gugu.
Kwa
upande wake Noel Bismark mwananchi aliyekwenda kupata huduma katika kliniki
hiyo alisema kuwa utaratibu ule ni mzuri kwa sababu una uwazi na uwajibikaji
tofauti na maafisa wanapofanyika kazi katika ofisi zao.
Kilini
ya Ardhi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilianza tarehe 16 mwezi huu na
itaendelea hadi tarehe 20 mwezi huu.
MWISHO
Comments
Post a Comment