Wenyeviti wa mitaa Dodoma wahimizwa kutoa huduma bora
Na. Halima Majidi, MTUMBA
Wenyeviti
wa mitaa jijini Dodoma wametakiwa kutambua na kusimamia majukumu yao ipasavyo
kwa kuwapatia huduma bora na kuwashirikisha wananchi katika miradi mbalimbali
ili kuleta tija katika ulinzi na utunzaji wa miradi hiyo.
Hayo
yalisema na Mwezeshaji wa Mafunzo ya Uongozi na Utawala bora, Mwinyipembe Victor,
wakati akitoa mafunzo hayo kwa wenyeviti wa mitaa yaliofanyika katika ukumbi wa
mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliopo Mji wa Serikali Mtumba.
Victor
alisema kuwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ndogo ya 146
dhumuni la kuwepo kwa serikali za mitaa nikupeleka madaraka kwa wananchi, hivyo
wenyeviti wa mitaa wanatakiwa kukumbuka na kutekeleza madaraka yao. “Wenyeviti
wa mitaa tumekuwa tunajisahau sisi tunakuwa mabosi halafu wananchi wanakuwa
wanahangaika, mwananchi atahangaika ndani ya miaka mitano ambayo umemnyanyasa
ila ipo siku na wewe utahangaika” alisema Victor.
Aidha,
aliwasitiza wenyeviti wa mitaa kutowaacha nyuma wananchi badala yake kuwachukulia
kama wao ndio waajiri wao kwa kutekeleza dhamana zao ikiwemo kuwatumikia na
kuwahudumia ipasavyo. “Lengo la kuwashirikisha wananchi katika miradi ya
maendeleo ni kutengeneza ari ya umiliki,
mwananchi akishirikishwa katika kupanga hata kwenye kulinda na kutunza lazima
atatekeleza tu, serikali ya mtaa itafanya vizuri endapo mwananchi atapewa madaraka yake” alisisitiza
Victor.
Sanjari
na hayo aliongeza kuwa moja ya majukumu ya serikali ya mtaa ni kuhakikisha
utekelezaji wa sheria za ulinzi wa wananchi pamoja na kuwepo kwa demokrasia
katika mitaa. Pia kazi ya serikali ya mtaa ni kuhakikisha wanasimamia taratibu
zote zinazohusu mpango mji.
“Kuna
sheria inayohusu urembeshaji miji hatuwaambii tu wananchi kuwa wapake rangi ili
mtaa upendeze hapana ni sheria inatutaka tuwe na utaratibu wa kuhakikisha mitaa
yetu inapendeza na kwa hapa Dodoma tumeanzisha utaratibu wa kuezeka bati la
rangi fulani ni kwaajili ya mtaa fulani. Haya yote ni majukumu ya serikali za
mitaa” aliongeza Victor.
Nae,
Mwenyekiti wa Mtaa wa Sogeambele, Kata ya Chihanga, Meshack Joseph, alisema
kuwa anashukuru kwa mafunzo kwasababu yamemfundisha kuwa na weledi katika
shughuli anazotakiwa kuzifanya. Pia yamemjengea uwezo wa kujiamini katika
utendaji wa kazi. “Kwasababu sehemu nyingine tulikuwa tunafanya kwa kupapasa
papasa kwa kujua kwamba nikifanya hiki nitakuwa nimekosea lakini kumbe baadhi
ya mambo tulikuwa tunaenda sawa lakini tulikuwa tunaenda kwa kutojiamini. Hivyo,
mafunzo haya yametujengea uwezo wa kujitambua, kama mwenyekiti majukumu yangu
ni yapi” alisema Joseph.
Alifafanua
kuwa katika mafunzo hayo alijifunza sehemu kubwa kuhusu namna ya kuwashirikisha
wananchi wake katika masuala mbalimbali yanayohusu mtaa wake ikiwemo utoaji wa
maamuzi. “Katika utekelezaji wa mambo yangu, cha kwanza kabisa nikufanya
taratibu za kuwashirikisha wananchi wangu katika maamuzi ya mambo yote
ninayotaka kwenda kuyafanya kwenye mtaa wangu na pia nitaangali taratibu
nyingine za kuibua miradi mbalimbali kwa manufaa ya wananchi wangu” alifafanua
Joseph.
Upande
wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Nyumba 300 Nzuguni, Donata Zitatu alisema kuwa, amefurahi
sana kwa mafunzo hayo, kwasababu yamemuwezesha kujua mipaka yake na utendaji
kazi kama mwenyekiti pamoja na kusimamia mtaa wake, pia amejifunza namna ya
kuanzisha vyanzo vya ndani vya mapato pamoja na kubuni miradi ya ndani
itakayowasaidia kuingiza mapato ya ndani. “Mambo mengi tulikuwa tunaenda tu
lakini semina ya leo imenisaidia na imenigusa sana, natoa shukrani zangu kwa wadau,
Mkuu wa Wilaya, Shekimweri pamoja na Mkurugenzi wa Jiji kwa kubuni semina hii
kwaajili yetu, kwasababu imetufundisha mambo mengi kama wenyeviti” alisema
Zitatu.
MWISHO
Comments
Post a Comment